KENYAN

 

Kwa ajili ya unganisho kwa YULE MTAKATIFU mbarikiwa ni YEYE na uwepo WAKE katika hofu, na upendo, kuunganisha jina la YAHUVEH YAHUSHUA na RUACH HAKODESH

Katika umoja kamili katika jina la Bi-arusi wa YAHUSHUA na Israel yote.

Tazama, tunakuja kutimiza amri ya Hanukkah sikukuu ya kuwekwa wakfu [kwa Hekalu].

Wakati wewe, YAHUSHUA ni nuru ya dunia, unakuja kutupatia uhai na nuru, tunajiweka wakfu upya kama hekalu wakati wa sikukuu ya kuwekwa wakfu [kwa Hekalu].

Na yawe mapenzi yako YAHUVEH MUNGU wetu, na MUNGU wa mababu wetu kwamba huu uwe wakati wenye kufaa mbele zako kwa ajili ya kuangalia kuasha taa ya Hanukkah: ni kama kwamba tulikuwa Tumeelewa siri zote za kustaajabisha ambazo zimefungiwa ndani yake.

Na ipae mbele yako na kusudi la hii amri kama inavyofanywa na watoto wa wapendwa wako ambao huweka wakfu na kufunza majina yenu matakatifu ambayo yanakumbushwa na nuru ya YAHUSHUA.

YAHUSHUA, ndiye nuru ya dunia ambaye hukuza kuunganishwa [na]  kulinganishwa viwili kwa sifa kuu na takatifu, na angaza kupitia uwepo wako wa uweza ile Mianga mikuu ili kuweze kuwa katika uanzilishi wa kuelekezwa kwetu, watumishi wako.

Maana ni wewe ungewasha taa yetu YAHUSHUA, MUNGU wetu ambaye utaangaza giza letu.

ABBA YAHUVEH Tuma nuru na ukweli wako kutuongoza kulicha, na kulipenda jina lako: kusoma na kufunza majina yako matakatifu na Torah takatifu, na unabii zako takatifu na uangalifu mkubwa, na kupeana heshima na utukufu kwa jina lako lililobarikiwa na kutukuzwa.

Kwa ajili ya uweza wa asili wa taa za Hanukkah tufanye wenye busara kupitia nuru ya dunia ambayo iligeuka mwili YAHUSHUA ha MASHIACH.

Na mstari huu utimizwe kama ulivyoandikwa “haitaondoka midomoni mwenu, midomoni mwa watoto wenu na midomoni mwa watoto wa watoto wenu” asema YAHUVEH “toka sasa hadi milele”

Na watoto wetu na wajukuu wawe wafuasi wa BWANA YAHUSHUA na Torah yake kama watu waaminifu, wapendwa juu na wahifadhiwa kwa upendo mkubwa chini, na utupe nguvu kuelekeza nafsi kwake YAHUSHUA yote kulingana na mapenzi yako.

Fungua macho yetu ili tuweze kutambua ajabu za YULE MTAKATIFU wako ili tujue nini tumaini la wito wake, utajiri wa urithi wa utukufu kwa Watakatifu, na kueleza ukweli na siri zake.

Katika ustahili wa YAHUSHUA MASIYA, Kuhani Mkuu, tuonyeshe maajabu na kupitia nuru yako na tuone nuru.

Takasa mioyo yetu kwa utumishi wako: tuweke mbali na maovu na mawazo Mageni. Na macho yetu yaone kurudi kwako Sayuni na rehema wakati utaziwasha tena hizo taa.

Tutakutumikia milele.

Na usemi wa midomo yetu na mawazo ya mioyo yetu yapate fadhila mbele zenu ABBA YAHUVEH, YAHUSHUA NA RUACH HA KODESH.

Kwa maana ombi letu ni kwako ABBA YAHUVEH. Kwa wakati unafaa, katika wingi wa fadhili zako tujibu na ukweli wa wokovu wako YAHUSHUA mwana wako wa pekee. Na furaha ya YAHUVEH, MUNGU wetu iwe juu yetu, Na Aimarishie kazi ya mikono yetu; kazi ya mikono yetu Na aimarishe, katika Jina la YAHUSHUA Ha MASHIACH tunaomba, Amen.



MAELEZO YA IMANI   Statement of Faith

Ombi la Wokovu   Salvation Prayer

Ombi la Wokovu katika Sauti 1



Ombi la Wokovu katika Sauti 2



1   2   3   4   5   6   7   8   9   10   12   30   31   33   36   37  
24 Sehemu ya 1   42   42   49   54   55   57   63   69   72   73   75   79   89   90   101   105   110   115   116   119   120   133   134